USAID DEC
Elimu ni haki ya kimsingi ya binadamu, na serikali ya Kenya imejitolea kuwapa wananchi wake elimu bora.
181 pages

Abstract
Raslimali nyingi zimewekezwa ili kuimarisha upatikanaji, umuhimu, usawa na ubora wa elimu. Serikali inatambua kwamba ili kuweza kushindana katika nyanja za kimataifa na kuimarika kiuchumi, taifa linahitaji elimu inayowawezesha wananchi kuwa wabunifu, kupata elimu ya kudumu maishani na wanaoweza kufanya kazi zilizo tata na zenye changamoto. Mabadiliko yamefanywa ili kuimarisha sekta ya elimu, na mifumo ya utafiti kama vile Tathmini ya Kitaifa na Ufuatiliaji wa Mafanikio ya Masomo (NASMLA) na Muungano wa Kusini na Mashariki mwa Afrika wa Kufuatilia Ubora wa Elimu (SACMEQ) inaonyesha kuwa kuna umuhimu wa kuboresha mafanikio katika uwezo wa kusoma na kufanya hesabu. Maendeleo yaliyofanyika hivi karibuni katika nchi ya Kenya yalionyesha kuwa kuna haja zaidi ya kuwa na mfumo wenye kina wa kuhakikisha ubora wa elimu. Mpangilio wa masomo katika kitabu hiki cha mwalimu uliandikwa ukizingatia mwongozo shupavu wa washauri wa kusoma na lugha kutoka hapa nchini Kenya na kimataifa. Mpangilio huu unazingatia sauti za herufi zinazotumika mara nyingi katika lugha ya Kiswahili na lugha ya Kiingereza. Kila mpangilio wa somo una mbinu mbalimbali zinazotoa mwelekeo wa kipekee wa kufunza kusoma kwa lugha ya Kiswahili. Mpangilio huu pia unasisitiza wazo kuu la kusoma na kuandika, na kuhakikisha kwamba wanafunzi wote nchini Kenya wanaweza kusoma na kuelewa ifikapo mwisho wa mwaka. Mpangilio huu unazingatia vipengele vinne vya lugha (kusikiliza, kuongea, kusoma na kuandika) na vipengele vitano muhimu vya kusoma: Utambuzi wa fonimu, utambuzi wa herufi, utambuzi wa maneno, kusoma kwa mtiririko unaozingatia shada na kiimbo na kusoma kwa ufasaha na kuelewa unachokisoma. Mpangilio huu unahakikisha kwamba wanafunzi wote nchini Kenya wanaweza kusoma na kuelewa ifikapo mwisho wa mwaka. Mpangilio huu unazingatia sauti za herufi zinazotumika mara nyingi katika lugha ya Kiswahili na lugha ya Kiingereza. Mpangilio huu pia unasisitiza wazo kuu la kusoma na kuandika, na kuhakikisha kwamba wanafunzi wote nchini Kenya wanaweza kusoma na kuelewa ifikapo mwisho wa mwaka.
Connected topics
Classification